TANZANIA: Raisi Magufuli atangaza baraza Jipya la Mawaziri

Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ametangaza baraza jipya la mawaziri leo tarehe 7/10 katika hafla fupi iiyofanyika ikulu na kuuzuliwa na makamu wa raisi pamoja na waziri mkuu ambapo wizara zimeongezeka kutoka wizara 19 hadi 21.

 
Kugawanya kwa wizara imetokana na wizara mbili kugawanywa huku akiongeza manaibu waziri kwa baadhi ya wizara.

Akitangaza baraza la mawaziri Raisi Magufuli amesema wizara ya nishati na madini ambayo ilikuwa ni wizara moja imegawanywa mara mbili, ambavyo kwa sasa kutakuwa na Wizara ya nishati na wizara ya madini

Akizungumza Raisi amesema lengo kubwa la kugawa wizara ya nishati na madini ni kutokana na umuhimu wa rasilimali hiyo kwa taifa na kwamba wizara zote hizi mbili zitakuwa na waziri na naibu wake.

Raisi ametaja mabadiliko mengine katika wizara ya kilimo, mifugo, na uvuvi ambavyo kwa sasa kutakuwa na wizara ya kilimo inayojitegemea na wizara nyingine itakuwa ni wizara ya mifugo na uvuvi.

Akiongea Ikulu Raisi Magufuli amesema sababu ya kufanya mabadiliko katika wizara ya kilimo, mifugo na uvivu kuwa wizara mbili tofauti ni kutokana na umuhimu wa sekta hii muhimu inayoajiri asilimia kubwa ya watanzania zaidi ya asilimia 75, kila wizara itakuwa na waziri na naibu waziri wake.

Mabadiliko mengine ni katika wizara ya Tamisemi baada ya kuwekewa manaibu waziri kwasababu ni wizara inayogusa sehemu kubwa ya wananchi.
Pia katika wizara ya Viwanda na biashara ameiongezea naibu waziri ili kuharakisha shughuli za kimaendelea tofauti na hapo mwanzo ambapo ilikuwa na waziri pekee.

Orodha ya mawaziri hii hapa


  • Wizara ya Ofisi ya Raisi Utumishi na Utawala bora
Waziri ---- George Huruma Mkuchika


  • Wizara ya TAMISEMI
Waziri ------  Suleiman Japho


  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
Waziri ------   Luhaga Mpina
Naibu Waziri -----  Abdallah Ulega


  • Wizara ya Maji na umwagiliaji
Waziri – Isack Kamwelwe
Naibu waziri – Juma Hamidu Aweso


  • Wizara ya habari, utamaduni, wasanii na michezo
Waziri – Dr. Harrison Mwakyembe
Naibu waziri – Juliana Shonza


  • Wizara ya afya, maendeleao ya jamii, jinsia, wazee na watoto
Waziri – Ummy Mwalimu
Naibu waziri – Faustine Ndugulile


  • Wizara ya Elimu, sayansi, Teknolojia na Ufundi
Waziri – Joyce Ndalichako
Naibu waziri – William Ole Nasha


  • Wizara ya viwanda, biashara, na uwekezaji
Waziri – Charles Mwijage
Naibu waziri – Stella Manyanya


  • Wizara ya Maliasili na utalii
Waziri – Hamisi Kinwangala
Naibu waziri – Ngailonga Josephat


  • Wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi
Wizara – William Lukuvi
Naibu waziri – Angelina Mabula


  • Wizara ya mambo ya ndani
Waziri – Mwigulu Nchemba
Naibu waziri – Hamad Masauni


  • Wizara ya Ulinzi na jeshi la kujenga taifa
Waziri – Dr. Hussein Mwinyi


  • Wizara ya katiba na Sheria
Waziri – Palamagamba Kabudi


  • Waziri wa mambo ya nje, ushirikiano wa afrika mashariki, kikanda na kimataifa
Waziri – Agustino Mahiga
Naibu waziri – Dkt Susan Kolimba


  • Wizara ya madini
Waziri – Angela Kairuki
Naibu waziri – Haroon Nyongo


  • Wizara ya nishati
Waziri – Medrad Matogoro Kalemani
Naibu waziri – Subira Hamisi Mgalu


  • Wizara ya Fedha na mipango
Waziri – Dr Philip Mpango
Naibu waziri – Dr Ashatu Kijaji


  • Wizara ya ujenzi, uchukuzi na mawasiliano
Waziri – Prof. Makame Mbarawa
Naibu waziri – Atashasta Nditiye
Naibu waziri – Eliasi John Kwandikwa


  • Wizara ya kilimo
Waziri – Charles John Tizeba
Naibu waziri – Mary Mwanjelwa


  • Wizara ya Waziri mkuu: Sera, bunge, kazi, vijana, ajira na walemavu
Waziri – Jenista Mhagama
Naibu waziri – Anthony Peter Mavunde
Naibu waziri walemavu – Stela Alex Likupa


  • Wizara ya ofisi ya makamu wa raisi, muungano na mazingira
Waziri – January Makamba
Naibu Waziri – Kangi Lugola
TANZANIA: Raisi Magufuli atangaza baraza Jipya la Mawaziri TANZANIA: Raisi Magufuli atangaza baraza Jipya la Mawaziri Reviewed by info tza on 12:15 PM Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.